
Posted on 13 April 2011
Siku za karibuni tulimskia C-pwaa wakati wa uzinduzi wa album yake akitangaza kuwa yeye na Suma lee wamerudi pamoja na kurudisha kundi kama Parklane lakini baada ya kupiga show ya uzinduzi na CP kwenye uzinduzi wake, leo Suma Lee ametoa mpya baada ya kudai kuwa CP hajamlipa pesa zake zote badala yake alimpatia nusu na kudai kuwa show haijafanya poa yaani haikumlipa, “kwanza alidanganya kuwa parcklane itarudi lakini sio kweli, Parklane irudi kwenye uzinduzi wake tu? Mwambieni kuwa hizo pesa alizonidhulumu kama ye anaona ni kidogo mi zinanitosha kwa kilo mbili za GOMBA” alisema Suma Lee
Baada ya habari hiyo kusambaa Cpwaa aliandika kwenye Facebook status yake; “So sad what i heard on the Radio today about my friend, i guess he got his message sent, Some people will never change! wishing him all the best!”