
Posted on 16 June 2011
Kifaa kipya cha bendi ya Kalunde, Bob Rudala mwishoni mwa wiki alikuwa kivutio katika maonesho ya bendi hiyo, yaliyofanyika ktk kumbi kadhaa jijini Dsm.
Bob Rudala ambaye awali alitamba na bendi ya In Afrika, aliwashika vilivyo mashabiki wa bendi hiyo waliohudhuria maonesho hayo haswa baada ya kuweza kwenda sambamba ktk nyimbo mpya za bendi hiyo za Fungua, Masumbuko na Sisee.
Licha ya kutamba na nyimbo hizo, Kalunde pia iliweza kutumbuiza nyimbo zao za zamani zilizopo katika albamu ya Hilda.
Akizungumzia ujio wa Rudala,Rais wa bendi hiyo Deo Mwanambilimbi alisema “Baada ya kumnasa Bob Rudala katika bendi yetu, hivi sasa tupo katika hatua za mwisho kukamilisha nyimbo nyingine tatu ambazo zitachanganywa na alizokuja nazo Rudala,” alisema Mwanambilimbi.
Habari na darhotwire