
Posted on 03 July 2011
Mcheza sinama za Bongo, Mariam Jolwa a.k.a Jini Kabula amekanusha kufunikwa na wasanii wanaochipukia kwenye tasnia hiyo wanaodaiwa kuigiza kuwa usitadi mkubwa kuliko yeye.
Jini Kabula alisema kuwa hayupo kwenye fani hiyo kwa ajili ya kushindana bali anatumia kipaji alichopewa na Mungu kufikisha ujumbe ambao hulenga kuufikisha katika jamii kupitia sehemu ambazo hucheza.
Aliendelea kufunguka kuwa, kilichomtambulisha katika fanii hiyo ni nafasi ya jini ambayo alifanikiwa kuicheza kwa ustadi na watu kuamini kuwa yeye ni jini kitu ambacho anadai hakiwezi kufutika haraka kichwani mwa watu.
“Kwenye tasnia ya filamu nilitambulika kama jini na hilo ndilo jina lililonitoa hivyo hakuna wa kunishinda ninajiamini na ninauwezo mkubwa wa kucheza kila sehemu ninayopewa kufanya hivyo, sipo kimashindano bali najivunia kipaji changu” alisema Jini Kabula.
Habari / Picha na GPL