
Posted on 20 February 2012
MSANII wa muziki wa kizazi kipya bongo,Heled, anayefananishwa na nyota kutoka marekani ‘TI’, amesema kuwa anaamini ipo siku atakuja kufanya kazi na nyota huyo ili kutimiza ndoto yake.
Msanii huyo amekuwa akifananishwa na nyota huyo kutoka Marekani, kitu ambachokinampa hamasa kubwa ya kukutana naye ili kurekodi pamoja.
Alisema kuwa katika albamu yake inayokuwa ambayo itakuwa ya kwanza anahitahi kufanya juu chini ili aweze kurekodi kazi moja na msanii huyo ili iwe kumbukumbu katika maisha yake ya muziki.
“Napenda siku moja nifanye kazi na T.I, kwani hayo ni malengo yangu ambayo yapo katika kichwa changu hivyo naamini kila kitu kitaenda sawa ,” alisema.
Na Laurent Samatta