
Posted on 09 April 2012
Mshindi wa kwanza, mrembo Like Abraham (kulia), akipokea hundi ya Shilingi milioni 10 kutoka kwa Mkurugenzi wa Global Publishers, Eric James Shigongo.

Mshindi huyo (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Wellu Sengo (kushoto) na mshindi wa tatu Zalha Sadallah.

Like (katikati) akiwa na majaji wa shindano hilo Salehe Ally (kulia) na Baby Madaha (kushoto).

Mkurugenzi wa Global Publishers, Eric Shigongo, akiwa na ‘Kina Rihanna’ kabla shindano kuanza.

Majaji wa shindano (kutoka kushoto) Salehe Ally, Baby Madaha na Eric Shigongo, wakiwa kazini.


Shabiki akiwasha mshumaa kumkumbuka mcheza sinema, marehemu Steven Kanumba.

Mchekeshaji Bambo akitoa burudani

Mchekeshaji Mtanga nae alitoa burudani kali

Like Abraham usiku wa kuamkia leo aliibuka kidedea katika shindano la ‘Vaa, Imba, Cheza kama Rihanna’ ambalo lilifanyika katika ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala jijini Dar es Salaam na kufanikiwa kujinyakulia Shilingi milioni 10. Kabla ya shindano hilo kulikuwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiwemo Bambo, Mtanga na H. Mbizo.
PICHA NA: RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY/GPL