“RAY C” ATAMANI KURUDI KWENYE UTANGAZAJI…!!
13 April 2012

Posted on 13 April 2012

MSANII wa muziki bongo anayefanya kazi zake Nairobi Kenya, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amedai kuwa anatamani kurudi nyuma na kuendelea na kazi yake ya awali ya utangazaji na u-Dj kwa madai kuwa bado anauwezo mkubwa na kazi hizo.

Akiongea na mwandishi wetu kwa njia ya mtandao, Ray C, anaamini fani hiyo ya utangazaji bado anaiweza hivyo anafikiria kurejea bongo na kuendelea na kazi hiyo katika kituo atakachoamua kuomba kufanya kazi.

Ray C, awali kabla hajaanza muziki alikuwa akitangazaji pia Dj, katika kituo cha redio Clouds FM akiwa na kipindi chake cha miziki ya Hip Hop, R&B na Taarab ambapo alichokipa jina la “Dr Beat”.

“Kuna watu hawajui kama mimi niliwahi kufanya kazi hii, lakini kazi yangu ya kwanza kufanya ilikuwa ndiyo hii tena baada ya kumaliza elimu yangu ya Sekondari tu,” alisema.

Hata hivyo anadai kuwa anapenda kujifunza zaidi U-Dj, kwani fani hiyo anayeipenda kuliko kitu kingine chochote ingawa si zaidi ya muziki anaofanya.

Na Laurent Samatta

Tags
< PREVIOUS POST
NEXT POST >
Most Read News

3 Comments

  1. George Mvungi says:

    Ray c, hata hivyo unafaa ilatatizo lako hurithiki ila mungu kama amekupangia kupata utapata tu nafatiliaga sana taarifa zako, Nairobi ulisema umepata kazi ya uwakala wa vinywaji naona umeona hailipi Rudi bongo Dada,

  2. anold says:

    RAY C,HAPO MAHALI ULPO SASA TAZAMA UPEPO WAKO UNAELEKEA WAPI KWA SASA KAMA KWENYE MUZKI UNAONA UMEPOTEA YA BD URUDI KWENYE KIPAJI CHAKO CHAUTANGAZAJI KWA SABABU UWEZO WA SAUTI NZURI NDO INAKUFANYA USHNDWE KUJUWA NKIPI CHA KUEKEZA KATKA LIFE LAKO LA UZEENI ,ME ANOLD NAKUSHAURI URUD KWENYE UTANGAZAJI MZKI UMEKUSHNDA DADA YANGU!!!!!!!!!MWSHO NAKUPA BG UP HAD KUFKA HAPO ULPO SASA ……….ILA MSHUKURU MUNGU ALYEKUPA UZURI ,SAUTI MURUWA TAMBUWA WAPO WA2 WANATAMAN WAWE KAMA WEWE ILA NDO IVO UMEPEWA WEWE TUMIA KIPAJI CHAKO KWA UANGALIFU!!!!!!!!!!!!

  3. fred godfrey says:

    eeeeeeeeh!kaz ipo ila 2nakukarbsh kweny hii tasnia ya habari na mawaslano kwan hata hvyo umrth ur c* mheshmwa Betty mkwasa


LEAVE A COMMENT

NOTE: To comment it is better that you have a gravatar account.
You can get a free gravatar account by clicking here.








SEARCH DARTALK

Copyright © 2011. DarTalk.com . All Rights Reserved. Site by NEXUS  |   BACK TO TOP!