
Posted on 16 April 2012
ANAPITA - BARUA KWA MAMA
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Anapita, msanii wa miondoko ya AfroFusion anayewakilisha chuga kaskazini mwa Tz, sasa aja na “Barua kwa Mama” aliyorekodi pande za noizmekah.com kwa defxtro, asema “wimbo huu nimeuandika kutokana na maisha ya mjini jinsi yalivyo, vijana wengi tumekuja kutafuta na mama zetu wako mbali na sisi, kwa jinsi maisha yalivyo wakati mwingine mshiko wa kumpigia mother hauna, na wakati mwingine mama mwenyewe kijijini hana simu mpaka kwa jirani, kuna wakati hawa wamama hudhani kwamba tumewasahu halafu huku mjini tunakula bata lakini si kweli, ni utaftaji hapa na pale changanyia na panda shuka ya gharama halisi ya maisha, pia kuna marafiki ambao kwa bahati mbaya mama zao washatangulia mbele za haki, nao hufikiria kuandika barua. Nawapenda mama zetu wote duniani kwa sababu natambua umuhimu wao.