
Posted on 18 May 2012
Wakameruni wapatao zaidi ya 5,000 waishio nchini ujerumani wanatalajia kujimwaga kujirusha na muziki wa dansi wa Ngoma Africa Band huko mjini Stuttgart, Ujerumani siku ya jumamosi 20 Mei 2012, katika sherehe maalum ya nchi yao “Cameroon Challenge” . Kamati ya maandalizi ya jumuhia ya wakameruni nchini Ujerumani imetoa mwaliko kwa bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa Band almaarufu FFU, kutumbuiza katika sherehe hizo zitakazo fanyika mjini Stuttgart, nchini Ujerumani, ambako zitahudhuriwa na wakameruni 5000 pamoja na wageni wa mataifa mbali mbali.
Mzimu huo wa dansi Ngoma Africa band aka FFU unatarajiwa kutoa burudani ya kuwapandisha mzuka wadau wote watakao jimwaga uwanjani, Ngoma Africa band sasa wanatamba na wimbo mpya “Uhuru wa Habari” sikiliza @ www.ngoma-africa.com