Posted on 05 July 2012
WAKATI wengine wakiamini kuolewa ni moja ya mafanikio katika maisha, msanii Jini Kabula, kwa upande wake amedai kuwa kuolewa ni moja ya njia ya kukaribisha umaskini kwani wanawake wengi hulazimika kuzaa hata kama hawajapanga.
Akizungumza na DarTalk msanii huyo alidai kuwa wanawake wengi wanaofunga ndoa huwa wanalazimishwa kuwa na watoto kabla ya kujipanga kuwa katika mazingiza mazuri ya kulea familia inavyostahili.
Alisema kuwa kwa upande wake hafikirii kuishi na mwaume kwani hataki kujizeesha mapema badala yake ataishi kwake hadi pale atakapoona maisha ya kibachela yamemshinda.
Tatizo wanawake wa kileo wanataka wawe last say ktk nyumba,sijui ndo utandawaz?