SHETTA, LADY JAY DEE NDANI YA NGOMA MOJA…!!
09 July 2012

Posted on 09 July 2012

BAADA ya kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Nidangaye’ msanii Shetta, amesema kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato mpya wa kufanya
ngoma na mwanadada Lady Jay Dee, lakini bado wanabishana juu ya kuipa jina ngoma hiyo.

Akizungumza na DarTalk, Shetta alidai kuwa mbali na kubishana juu ya jina la ngoma yake kwa upande wake anaamini itaitwa ‘Bonge la Bwana’, ingawa hajataka kueleza maana halisi ya neno na maneno yatakayotumika.

Msanii huyo alisema kuwa kitendo cha kufanya ngoma na Lady Jay Dee ni kutokana na kumkubali mwanadada huyo nguli wa muziki tanzania kwani ana imani ngoma hiyo itakua nzuri kutokana na sauti yake.

“Baada ya ngoma yangu ya ‘Nidanganye Danganye’ kufanya vizuri kwa sasa nipo na Lady Jay Dee nataka kufanya naye ngoma ambayo najua itafanya vizuri hivyo mashabiki wangu naomba wakae mkao wa kula,” alisema Shetta.

Tags ,
< PREVIOUS POST
NEXT POST >
Most Read News

One Response

  1. HAMZA KAMBI says:

    Mambo vipi m2 mzima, mimi ni bongo la shabiki wako kwani nazikubali sana kazi zako uko juu mazazi kwa makamuzi hayo usirudi nyuma endelea kulisongesha gurudumu la bongo frever, kandamiza mwana mpaka mwisho umetisha mbayaaaa, Tunaisubili hiyo kazi utakayomshilikisha mwanadada mkari wa voko. BIG UP MEN.


LEAVE A COMMENT

NOTE: To comment it is better that you have a gravatar account.
You can get a free gravatar account by clicking here.








SEARCH DARTALK

Copyright © 2011. DarTalk.com . All Rights Reserved. Site by NEXUS  |   BACK TO TOP!