
Posted on 18 September 2012
WAKATI wasanii wengine wakitupilia mbali mawazo ya kutoa albamu kwa madai kuwa hazina soko na wanaibiwa sana msanii anayetesa na ngoma yake ya ‘Thamani Yetu’, H-Baba, amesema kuwa anatarajia kuachia albamu yake Novemba mwaka huku ikiwa imepewa jina la ‘Shika Hapa Acha Hapa’, itakayokuwa na nyimbo 10.
H-Baba alizitaja baadhi ya nyimbo zitakazokuwa ndani ya albamu hiyo kuwa ni pamoja na ”Thamani Yetu, ‘Shika Kichwa’, ‘Huendani Nami’, ‘Nipe Kidogo’, ‘Shika Hapa Hacha Hapa’ na nyingine kibao ambazo hajawahi kuziachia.
Alisema kuwa kwa upande hataki kusikiliza maneno ya watu kuwa albamu hazifanyi vizuri skoni kwani kila mtu anafanya anachojua na hakuna msanii anayetangaza kuwa albamu yake haijafanya vizuri.
“Wasanii wengi wanalalamika kuwa albamu hazifanyi vizuri nachoweza kusema ni kwamba kulalamika kwa mtu fulani hakuwezi kiunifanya mimi nishindwe kufanya kazi zangu za kila siku, albamu nitatoa na naamini mashabiki wataipokea na itafanya vizuri,” alisema.
Hata hivyo aliongeza kuwa baada ya ngoma yake hiyo ya ‘Thamani Yetu’, ambayo inafanya vizuri kwenye vituo vingi vya televisheni soon atakuja na kitu alichomshirikisha msanii wa muziki wa dansi Banza Stone ambaye hivi sasa yupo katika bendi ya Extra Bongo.