Posted on 20 September 2012
MSANII ndani ya tasnia ya filamu na tamthilia pia ni mkurungezi wa kampuni ya Tuesday Entertainment, ambaye ni wa baba wa mtoto Salma Tuesday, Mr Chuzi ametoa masikitiko yake kuwa kuna uwezekano mkubwa mama wa mtoto wake huyo Jini Kabula akamuharibu mtoto kwa kile kinachodaiwa kuwa hajatulia.
Akizugumza na DarTalk, Mr Chuzi ingawa hakutaka kufunguka sana, alidai kuwa zipo ishu ambazo zinaweza kumfanya akawa na wasiwasi kutokana na nyenendo za Kabula, kwani mtoto huchukua tabia nyingi kutoka kwa mama yake hasa msichana.

Mtoto wa Chuzi, Salma Tuesday
“Mtoto anaharibika kutokana na tabia za mama au baba hivyo wasiwasi wangu ni kwamba endapo Kabula hatobandilika sasa na kujua kuwa ana mtoto mkubwa ambaye anahitaji kukua kwenye maandili mema basi anaweza kumuharibu na mimi siwezi kukubali kitu hicho kitokee kwa mwanangu,” alidai.
Hata hivyo anaamini kuwa anaamini kila mtoto wa kitanzania endapo asingelelewa katika maandili mazuri basi taifa la leo lingekuwa kwenye matatizo makubwa.
bro mbona hofu we kauka tu